skip to Main Content
P.O. Box 65001, MUHAS,Dar es Salaam webmaster@muhas.ac.tz 0752360543 / 0756265177 - Admission Office
Kaimu Makamu Mkuu wa Chuo, Prof. Appolinary Kamuhabwa akimkabidhi tuzo kama ishara ya shukrani Prof. Eligius Lyamuya kwa uongozi mahiri wa kuandaa data za uanishaji wa ubora wa Vyuo Vikuu
Kaimu Makamu Mkuu wa Chuo, Prof. Appolinary Kamuhabwa akimkabidhi tuzo kama ishara ya shukrani Dr. Rehema Chande Mallya kwa uongozi mahiri wa kuandaa data za uanishaji wa ubora wa Vyuo Vikuu
Prof. Eligius Lyamuya akielezea uzoefu wake katika zoezi la kuandaa data kwa ajili ya uanishaji wa ubora wa Vyuo Vikuu unaofanywa na mtandao wa kimataifa wa Times Higher Education (THE)

Dr. Rehema Chande akielezea mchakato mzima wa kukusanya na kuandaa data kwa ajili uanishaji wa ubora wa Vyuo Vikuu unaofanywa na mtandao wa kimataifa wa Times Higher Education (THE)

Viongozi mbalimbali wa MUHAS wakifuatilia hafla fupi ya kuwapongeza Prof. Eligius Lyamuya na Dr. Rehema Chande Mallya
Kaimu Makamu Mkuu wa Chuo Prof. Appolinary Kamuhabwa (katikati), Kaimu Naibu Makamu Mkuu wa Chuo Taaluma, Prof. Emmanuel Balandya (kushoto) na Naibu Makamu Mkuu wa Chuo, Mipango, Fedha na Utawala, Prof. Erasto Mbugi (kulia) wakiwa katika picha ya Pamoja na Prof. Eligius Lyamuya na Dkt. Rehema Chande Mallya mara baada ya kukabidhiwa tuzo zao.

Tarehe 25 Agosti, 2023
Uongozi wa Chuo Kikuu cha Afya na Sayansi Shirikishi Muhimbili (MUHAS), leo umewapongeza Prof. Eligius Lyamuya na Dr. Rehema C. Mallya kwa uongozi wao mahiri kwenye zoezi la kuandaa na kuwasilisha data kwenye mtandao wa kimataifa wa Times Higher Education (THE) na hivyo kuiwezesha MUHAS kuwa miongoni mwa Vyuo Vikuu vitatu bora katika nchi za Kusini mwa Jangwa la Sahara.
Akizungumza katika hafla hii ya kuwapongeza, Kaimu Makamu Mkuu wa Chuo, Prof. Appolinary Kamuhabwa amewashukuru viongozi hawa kwa kazi kubwa waliyoifanya ambayo matokeo yake yameweza kukipatia Chuo sifa kubwa ndani na nje ya nchi. Pia amempongeza na kumshukuru Prof. Lyamuya kwa kuendelea kuwa mshauri (mentor) mzuri hapa Chuoni kwenye masuala la taaluma na masuala ya uongozi
Aidha Prof Kamuhabwa amewaomba wakuu wa ndaki, shule kuu, kurugenzi, idara na vitengo mbalimbali Chuoni watoe ushirikiano wa karibu na haraka pale data zitakapohitajika tena kwa ajili uanishaji wa ubora wa Vyuo Vikuu utakaofuata. Kaimu Makamu Mkuu wa Chuo pia amesisitiza umuhimu wa usahihi wa taarifa zinazowasilishwa kwa ajili ya uanishaji wa ubora.