skip to Main Content
P.O. Box 65001, MUHAS,Dar es Salaam webmaster@muhas.ac.tz 0752360543 / 0756265177 - Admission Office
Mkuu wa Kitengo cha Programu ya Jinsia Dkt. Hawa Mbawala akitoa semina kwa wanafunzi
Mkuu wa Kitengo cha Kudahili Ms. Renista Mkoba akiwaeleza wanafunzi kuhusu programu zinazotolewa MUHAS na vigezo vyake
Wanafunzi wakimsikiliza mtoa mada wakati wa semina chuoni hapo
Wanafunzi wakimsikiliza mtoa mada wakati wa semina chuoni hapo
Wanafunzi wakimsikiliza mtoa mada wakati wa semina chuoni hapo
Afisa Mwandamizi Tehama, Andrwe Katemi akitoa mada kuhusu TEHAMA
Mwanafunzi akiuliza swali wakati wa semina ya mwongozo wa fani ya afya na sayanshi shirikikishi
Mwanafunzi akiuliza swali wakati wa semina ya mwongozo wa fani ya afya na sayanshi shirikikishi
Wanafunzi wakipata chakula cha mchana baada ya semina ya fani ya afya na sayansi shirikishi iliyofanyika chuoni, MUHAS
Wanafunzi wakipata chakula cha mchana baada ya semina ya fani ya afya na sayansi shirikishi iliyofanyika chuoni, MUHAS

MUHAS kupitia kitengo cha Programu ya Jinsia (Gender Program Unit) wamefanya semina ya mwongozo wa fani za afya na Sayansi Shirikishi kwa wanafunzi wa kike wanaosoma mchepuo wa sayansi (PCB na PCM) kwa shule za sekondari ili kufahamu kwa undani kuhusu fani za afya na kuwaongoza katika  kufanya maamuzi ya fani wanazozitaka kusoma hapo baadae.

Mafunzo hayo yametolewa na Mhadhiri Kutoka MUHAS, Dkt. Hawa Mbawalla ambaye pia ni Mkuu wa Kitengo cha Programu ya Jinsia (Gender Program Unit) ambapo wanafunzi walipata elimu na muongozo wa kufikia ndoto za kuwa madaktari, wauguzi, wafamasia, madakatari wa meno, wataalamu wa maabara, wataalamu wa elimu ya jamii,  jinsi ya kuchagua fani, jinsi ya  kujiendeleza kitaaluma au fani na majukumu ya mwanafunzi wa masomo ya afya na sayansi shirikishi.

Vile Vile Mkuu wa Kitengo cha Udahili, Bi. Renista Mkoba aliwaelezea wanafunzi programu mbalimbali za afya na sayansi shirikishi zinazotolewa MUHAS na vigenzo vyake kuanzia ngazi ya Diploma mpaka Digrii na kuwasisitiza kusoma kwa bidii na malengo kulingana na fani wanazotaka kuchagua,

Naye Afisa mwandamizi wa TEHAMA, Bw. Andrew Katemi alitoa  mada  kuhusu umuhimu wa TEHAMA katika fani za afya na kuwasisitizwa wanafunzi kuwa wabunifu ili waweze kutatua changamoto zinazokabili jamii kupitia TEHAMA ambapo ndiyo dunia ya sasa ilipo na inapoelekea kwa kasi.

Mafunzo hayo  yaliweza kuhudhuriwa na wanafunzi kutoka Baobao, St. Francis Girl’s, Cannosa, Loyola, Ifunda Tech, Jangawani, Al Muntazir, Hopac, Heritage, Pandahil, Marian Girls, Almis, Babro Johson, Ifakara, Msolwa Girls, Korogwe Girls, na Mazinde na pia wanafuzi walipata fursa ya kuuliza maswali na kuwashukuru watoa mada kwa kuwapa elimu  ambayo imewasadia kufahamu kwa undani kuhusu fani za afya na sayansi shirikishi na itawaongoza katika kufanya maamuzi sahihi ya kuchagua fani wanazotaka.